Tuesday, May 24, 2016

JINSI YA KUPUNGUZA AU KUONGEZA UKUBWA WA MANENO KWENYE WHATSAPP

Wapo watu wengi ambao wanapenda kubadili ukubwa wa maneno kwenye baadhi ya app zilizopo kwenye simu zao. Siku ya leo tutatumia whatsapp kama mfano maana ndio app inatumiwa na watu wengi.

Siku chache zilizopita tulijifunza jinsi ya kuongeza ukubwa wa maneno au kupunguza ukubwa wa maneno kwenye simu yako ya android. Leo tutaona jinsi ya kupunguza au kuongeza ukubwa maneno na muoenekano kwenye baadhi ya apps utakazo taka.

NOTE

Unaweza tumia huu mfano kubadili muonekano wa ukubwa wa vitu kwenye app yeyote kwenye simu yako ya android.

STEP 0

Hakikisha simu yako tayari ume root. Kama hauja root simu yako basi hautaweza kufanikiwa kupunguza au kuongeza ukubwa wa maneno kwenye whatsapp.

STEP 1

Hakikisha kwenye simu yako tayari umeweka Xposed Installer. Xposed installer ina muonekano kama picha chini

STEP 2

Hakikisha ume intsall App setting Module. Kama bado unaweza ku-download kwa kutumia link chini kisha install kwenye simu yako
http://dl-xda.xposed.info/modules/de.robv.android.xposed.mods.appsettings_v29_70ccc5.apk

STEP 3

Baada ya kumaliza ku install App setting nenda kwenye xposed installer kisha nenda kwenye kipengele cha module na weka tick pembeni ya app settings kama picha chini kisha zima na kuwasha simu yako

STEP 4

Hakikisha Xposed installer imeruhusiwa kupata root ya simu yako. Kwa kizungu ni kwamba "make sure xposed installer has been granted root access to system files". Kwa kifupi fungua super user app halafu hakikisha xposed installer inafanana kama picha chini

STEP 5

Fungua App settings app kwenye simu yako na utapata muonekano kama picha chini

STEP 6

Shuka chini mpaka utakapo ona Whastapp kama picha inavyo onekana chini.

STEP 7

Bonyeza hicho kipengele cha Whatsapp kisha weka on kwenye neno setting kama picha inavyo onekana chini

STEP 8

Ebdapo utafanikiwa basi utapata muonekano kama picha chini

STEP 9

Kwenye sehemu iliyoandikwa DPI andika number yeyote mfano 320, 240... etc.. jinsi namba inavyozidi kuwa ndogo utakuwa unapunguza ukubwa wa maneno na muonekano wa whatsapp na jinsi unavyo andika number kubwa basi maneno na muonekano wa whatsapp utaonekana mkubwa.

STEP 10

Baada ya kuandika number unayotaka kwenye sehemu ya DPI (mfano mimi nimeandika number 250),bonyeza sehemu yenye alama ya save na utapata muonekano kama picha chini kisha bonyeza ok

STEP 11

Bonyeza sehemu iliyoandikwa MORE juu kulia kisha bonyeza kipengele kinachosema settingskama picha chini

STEP 12

Bonyeza kipengele kinachosema FORCE STOP kama picha chini

STEP 13

Zima simu yako kisha iwashe (restart). Nenda kafungue whatsapp na utaona muoenekano wa maneno na vitu vingene kwenye whatsapp vimebadilika. Mfano picha kushoto ni muonekano wa Whatsapp kabla sijaweka number kwenye DPI na picha kulia ni baada ya kuandika number 250 kwenye DPI.


Mpaka hapo tumefikia mwisho na kama umependa kazi zetu unaweza kutufwata kwenye instagram kupitia phonetricktz au wasiliana nasi kupitia whatsapp +255627732383.

No comments:

Post a Comment