Wednesday, June 17, 2015

NANI ZAIDI KATI YA LG G4 Vs SAMSUNG GALAXY S6


LG G4 na Samsung Galaxy S6 ni top smartphones ambazo zimetoka mwaka huu. Simu hizi mbili zina chuana vikali kila kona kuanzia kwenye screen, sound, camera, software etc. Leo tutachambua mambo manne ambayo ni Display, Software, Design na Camera

Display

Kwenye upande wa Display, Samsung Galaxy S6 ina beba kioo chenye ukubwa wa 5.1-inch Super AMOLED kikiwa na resolution ya 2560×1440 pamoja na 577ppi wakati LG G4 ina beba kioo chenye ukubwa wa 5.5 inch kikiwa na resolution ya 2560×1440 na 538ppi (pixels per density). Hapa tunaweza kuona LG G4 ina kioo kikubwa kushinda Samsung Galaxy S6 lakini kioo cha samsung ndio bora na pia unaweza kutumia S6 bila matatizo hata ukiwa nje kwenye mwanga wa jua.

Design na Hardware

Kwa upande wa Design na Hardware, Lg G4 inatumia chip ya Qualcomm Snapdragon 808 ambayo ni 64bit ARM wakati Samsung S6 ikitumia Exynos 7 Octa 7420 64bit ARM. Simu zote mbili zina RAM yenye ukubwa wa 3GB na uwezo wa LG G4 wa kubeba vitu ni 32GB wakati Samsung S6 ni 128GB.

LG G4 inakupa uwezo wa kutumia memory card wakati Samsung S6 haikuruhusu kuweka memory card. Battery ya LG G4 ina ukubwa wa kiasi cha 3000 mAh wakati Samsung S6 ina ukubwa wa kiasi cha 2600 mAh. Battery ya S6 haitoki wakati ya LG G4 inatoka huku ikiwa na uwezo wa kutumika kwa mdaa mrefu kushinda ya Samsung S6

Camera

Simu zote mbili zinakuja na camera ya nyuma yenye ukubwa wa 16 megapixels. Camera ya mbele ya LG G4 ni 8 megapixels wakati ya Samsung S6 ni 5 megapixels. Simu zote hizi mbili zinachuana vikali kwenye Camera na zote kwakifupi zinatoa picha na video zenye ubora.

Software

Simu zote mbili zinatumia android huku Samsung ikiwa inakuja na features kama Multi-window, Themes na Toolbox. Kwa upande wa LG G4 pia inakuwezesha kutumia multi-window, kuongeza na kupunguza ukubwa wa keyboard. Simu zote mbili zinachuana vikali kwenye software na kwa mtazamo wangu nadhani LG G4 yupo vizuri kwenye swala la software.

Hitimisho

Simu zote mbili ni nzuri na zote zina ubora mzuri na pia zinafaa na zinajitosheleza kutumika kwa mahitaji yako ya kila siku.

No comments:

Post a Comment