Saturday, March 26, 2016

JINSI YA KU UPDATE TECNO C8 ILI KUTUMIA MFUO MPYA WA HIOS

Baada ya watumiaji wa simu za Tecno kulalamika sana kuhusu kutopata update kwenye simu zao sasa Tecno wameamua kuanza kutoa update na amabo wataanza kufaidika ni wale wenye simu ya Tecno camon C8. Kwa wale wenye Tecno camon C8 hii ni habari njema kwenu kwa kuwa nitatoa maelekezo jinsi ya ku update simu yako ya Tecno Camon C8 ili uweze kuanza kutumia mfuo mpya ambao Tecno wanataka kuanzisha unaoitwa HIOS.

Kwanza nianze kueleza maana ya HIOS. Hios ni style mpya ambayo itakuwa inawekwa kwenye simu zote za Tecno. Mfano kwenye Samsung tuna Touchwiz, kwenye HTC tuna sense. Hios inakuja na mabadiliko mengi sana kwenye simu za Tecno. Moja ya vitu vichache ambavyo vitakuwa kwenye HIOS ni Fonts, Pop Incoming Call, Hi-Manager na mambo mengine mengi. Ili kujua jinsi Hios itakavyo kuwa basi bonyeza link chini
http://phonetricktz.blogspot.com/2016/03/hios-mfumo-mpya-wa-tecno-kipi.html

Leo nitatoa malekezo ambayo yatakusaidia kuweza ku update Tecno Camon C8 ili uweze kujua jinsi Hios itakavyokuwa pindi itakotolewa rasmi na Tecno siku chache zijazo.

Vigezo na Masharti

  • 1: Hakikisha simu yako ni Tecno Camon C8
  • 2: Hakikisha simu yako ina charge kuanzia 70%
  • 3: Hakikisha simu yako ina Memory Card
  • 4: Soma maelekezo yote kwa makini kisha ndio ujaribu kwenye simu yako

JINSI YA KU UPDATE TECNO C8 ILI KUTUMIA MFUO MPYA WA HIOS

STEP 0

Download update kulingana na toleo lako la C8. Ili kujua toleo lako la C8 inabidi uwende kwenye about phone kisha soma build number halafu angalia build number inayofanana na yako chini kisha bonyeza au click ili download. Tadhali Usi download build number ambayo haifanani na ile iliyopo kwenye simu yako maana unaweza haribu simu yako

STEP 1

Baada ya kumaliza ku download extract hilo file na ndani yake utakuta mafile mawili kama picha inavyo onekana chini. Mfano kama umedowload file kama hili OTA Package C8-H352-A2-L-20…60315.zip lifungue kwa kutumia es file explorer kwenye simu yako au kama unatumia computer lifungue kwa kutumia Winrar au 7zip program ili upate file linaloitwa update.zip.



Note
Usipo fanya hivyo basi hautaweza ku update simu yako. Hakikisha umefanya kama nilivyo eleza hapo juu

STEP 2

Baada ya kumaliza kufungua file ulilo download ili upate file linanoitwa update.zip kama picha inavyo onekana juu. Copy hilo file linaloitwa update.zip kwenda kwenye memory card ya simu yako.

STEP 3

Zima simu yako ya Tecno Camon C8. Kisha washa simu yako kwenye recovery mode. Ili kuwasha simu yako kwenye recovery mode unatakiwa ushikilie cha kuwashia na cha kuongeza sauti kwa pamoja na usiviachie mpaka simu yako itakapo onyesha logo ya Tecno kwenye display ndipo uviachie kama picha inavyo onekana chini

STEP 4

Subiri mpaka utakapo ona simu yako inafanana kama picha chini,



kisha bonyeza na kushikilia cha kuwashia kama sekunde mbili halafu bonyeza cha kuongezea sauti huku ukiwa umeshikila cha kuwashia na utapata muonekano kama picha chini. Kama ujapata muonekano kama picha chini rudia tena

STEP 5

Bonyeza cha kupunguza sauti mpaka utakofika kipengele kinachosema apply update from Sdcard kisha bonyeza cha kuwashia halafu bonyeza cha kupunguza sauti mpaka utakapofika kwenye lile file linaloitwa update.zip kama picha inavyo onekana chini

STEP 6

Bonyeza cha kuwashia kisha subiri kama dk 2-3 mpaka simu yako itakapo maliza ku update. Baada ya kumaliza simu yako itajiwasha yenyewe kama isipo jiwasha basi nenda kwenye kipengele kinachosema reboot system kisha bonyeza cha kuwashia.

Mpaka hapo utakuwa umefanikiwa ku update simu yako ya Tecno Camon C8 na utakuwa tayari umeanza kujionea jinsi Hios itakavyokuwa kwenye simu yako. Kagua simu yako kuona mambo yaliyo ongezeka. Kama umependa kazi zetu unaweza kutufwata kwenye instagram kupitia phonetricktz

Tembelea link chini kujua jinsi ya kuweka mfumo mzima wa Hios pamoja na Android 6.0 (Marshmallow) kwenye Tecno Camon C8
http://phonetricktz.blogspot.com/2016/04/jinsi-ya-ku-update-tecno-camon-c8.html

No comments:

Post a Comment