Tuesday, October 11, 2016

JINSI YA KUTENGENEZA APP YA BLOG KAMA YA MILLARDAYO.COM

Millardayo.com ina milikiwa na mtangazaji wa clouds maarafu kama Millardayo. Huyu jamaa anatangaza kipindi cha amplifier pia ni kijana anaye jishughulisha sana na mambo ya mtandao pamoja na technology. Vijana wengi wanatumia millardayo.com app kwenye simu zao lakini ni wachache sana ambao huwa wanajiuliza jinsi ya kutengeneza app kama ya millardayo.com.

Kabla ya kuanza kujifunza jinsi ya kutengeneza app kama ya millardayo.com ni vyema tujikumbushe kwanza masomo yaliyopita. Kwa wale ambao bado hawajajifunza jinsi ya kutengeneza android app part 1 na part 2 basi tembelea part 1 na part 2 chini
Fungua Android Studio kwenye computer yako. Kama hajui android studio ni kitu gani basi tembelea hizo link mbili juu kujua namna ya kuweka android studio. Kwa wale ambao wana android studio tayari, utapata muonekano kama picha chini



Kwenye application Name(Jina la app) andika Millardcopy
Company Domain andika phonetricktz.blogspot.com
Project location kwangu ni C:\Users\hubert\AndroidStudioProjects\Millardcopy. Kama unataka kuchagua sehemu nyingine ambapo unataka app yako ikae basi mbele kabisa ya kibox cha project location utaona vidoti vitatu vibonyeze kisha chagua ikae wapi app ya Millardcopy.
NOTE
Ni vyema ukatambua folder ambalo litakuwa linatumiwa na android studio kuhifidhi app yako ya Millardcopy.
Baada ya kumaliza bonyeza Next kwenye program yako ya android studio na utapata muonekano kama picha chini



Hakikisha kipengele cha Phone and Tablet umechagua Minimum SDK kuwa API 19: Android 4.4 (kitkat). Hii ina maanisha kwamba, app tunayotengeneza (Millardcopy) itakuwa inafanya kazi kwenye simu zizazotumia android 4.4 na kuendelea. Haikisha android studio kwenye computer yako ina fanana na picha yangu hapo juu. Kisha bonyeza Next kisha utapata muonekano kama picha chini



Bonyeza sehemu inayosema Basic Activity kama inavyo onekana kwenye picha juu. Zipo activity mbali mbali lakin sisi tutatumia basic activity kwa leo. Activity ni kama UI (user interface) nikimaanisha muonekano wa app ya millardcopy utakavyokuwa kwa mtumiaji. Baada ya kuchagua Basic Activity bonyeza Next na utapata muonekano kama picha chini



Chini kabisa, bonyeza sehemu inayosema finish kisha subiri mdaa mchache wakati android studio ikiwa inakuandilia muonekano wa app yetu ya Millardcopy. Endapo utafanikiwa utapata muonekano kama picha chini.



Kwa leo tuishie hapa. Kama unataka kuendelea na hili somo bonyeza Part 4 chini. Kwa wale ambao walikosa masomo yetu yaliyopita basi bonyeza part 1 kujua tulipo anzia.

Kama umependa kazi zetu usiache kutufwata kwenye instagram yetu ya phonetricktz au bonyeza picha chini kutembelea instagram yetu

1 comment: