Friday, January 29, 2016

JINSI YA KUIFANYA GALAXY S5 IWE NA SCREEN YA PEMBENI KAMA YA S6 EDGE PLUS

Wengi wetu tutakuwa tunaijua Samsung Galaxy S6 Edge plus kutoka na uzuri wake pamoja na umbo la kioo chake. Moja ya kitu kizuri ambacho kipo kwenye Galaxy S6 Edge ni uwezo wa kupata taarifa kama missed calls ambazo zinakuwa zinaonekana pembeni huku zikiwa rangi tofauti tofauti.

Leo tutaona jinsi ya kuifanya Galaxy S5 (SM-G900P) iwe na uwezo wa kutoa taarifa mbalimbali pembeni ya kioo kama ilivyo kwenye Galaxy S6 Edge Plus. Endapo utafanikiwa kufwatilia maelekezo yangu vizuri basi simu yako ya Galaxy S5 itakuwa ina uwezo wa kufanya mambo makubwa kama vile unatumia S6 edge plus.

JINSI YA KUIFANYA S5 IWE NA SCREEN YA PEMBENI KAMA YA S6 EDGE PLUS

STEP 0

Hakikisha tayari umeweka custom recovery kwenye Samsung Galaxy S5. Kama bado tembelea link chini kujua jinsi ya kuweka custom recovery kwenye Samsung Galaxy S5 (SM-G900P)
http://phonetricktz.blogspot.com/2015/11/jinsi-ya-kuweka-custom-recovery-kwenye.html

STEP 1

Tembelea link chini ili kujua jinsi ya kuibadilisha Galaxy S5 iwe na muonekano kama Galaxy Note 5 pia itumie android 5.1.1
http://phonetricktz.blogspot.com/2015/12/jinsi-ya-kuweka-android-511-kwenye.html

STEP 2

Baada ya kumaliza step 1, nenda kwenye settings kisha bonyeza kipengele kinachosema Edge screen na utapata muonekano kama picha chini

STEP 3

Bonyeza kipengele kinachosema People edge kisha hakikisha una ki turn on juu upande wa kulia kama picha chini

STEP 4

Baada ya hapo chini kidogo bonyeza kipengele kinachosema My people kisha chagua contact za watu wako wa nguvu ambao ungependa watokee pembezoni kwenye kio chako cha S5

Note
Endapo utapata missed call yoyote kutoka kwa hao watu ambao umewachagua basi missed call zao zitakuwa na muonekano kama picha chini.

STEP 5

Endapo utakuwa unataka pia apps unazotumia mara kwa mara zikae pembezoni mwa kioo basi nenda kwenye kipengele kinachosema Apps edge kisha chagua apps unazotaka. Kwa mfano mimi nimechagua apps ambazo zinaonekana kwenye picha chini





Kama umeshindwa kufwatilizia malekezo yetu na ungependa S5 yako iwe na uwezo kama wa S6 edge plus unaweza wasiliana nasi kupitia namba +255753877552 na gharama isiyopungua Tsh 25000 utatakiwa kulipa.

Kama unapenda kazi zetu unaweza ukatufwata kwenye instagram kupitia phonetricktz.

No comments:

Post a Comment